Thursday, October 25, 2007

HIVI NDIO MAMBO YALIVYOKUWA SIKU YA USIKU WA MWAFRICA ULIONDALIWA NA WENZETU WAMAREKANI

Shahili lifuatalo hapo chini liliimbwa pamoja na ngoma za kitamaduni zilitumbuizwa na wana SERA . Kama kawaida wana SERA waliendelea kulitangaza taifa lao jinsi lilivyo na vivutio vingi kwa watalii.Pia waliweza kuwafaamisha watu wote waliofika katika sherehe hizo jinsi Tanzania ilivyo nchi ya Amani na jinsi gani imekuwa ikisaidia nchi jirani katika maswala mabali mabali likiwemo lile la kusaidia sana katika kuifadhi wakimbizi.Mungu ibariki Tanazania
Mtunzi na mwandishi wa shahili hili ni mTanzania mwenzetu
Ndugu Freddy Mwisomba.

1) Tunaanza na salamu, Kwa wote mliofika,
Tunachukua jukumu, Kuwapa habari njema,
Sisi tuliopo huku, Ni wana wa Tanzania.
Nchi yetu Tanzania,Twawakaribisha wote.

2) Nchi yetu Tanzania,Ni nchi yenye Amani
Watu wake wakulima, Pia na wafanyakazi
Watoto wana furaha, Tamaduni zake safi.
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.

3) Watu wote mliopo, Mnaujua mlima,
Mlima Kilimanjaro, Upo kwetu Tanzania
Wasimama kama nguzo, Imara ya Africa.
Nchi yetu Tanzania,Twawakaribisha wote.

4) Ziwa kubwa Africa, Ni ziwa Victoria
Lipo kwetu Tanzania, Kenya pia na Uganda
Ni kivutio kikubwa, Wote mje kukiona
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.

5) Mbuga zetu za wanyama, Zapendwa na watalii,
Mikumi pia Manyara, Simba, Faru watawala,
Wapatikana Wanyama, Adimu kwenye dunia,
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.

6) Mira za Watanzania, Zimejengwa kwa busara,
Mdundiko Bongo fleva, Ngoma zetu tunacheza
Mbalimbali makabila, Kiswahili twazungumza
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.

7) Twapendana na wenzetu, Wakenya na Waganda
Biashara kwenda juu, Maendeleo makubwa,
Ushirikiano huu, Unaendelea sana,
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote

8) Si kama Tunajigamba, Ila Twasema ukweli
Mungu ametujalia,Nchi yetu ya Amani,
Aridhi yenye rutuba, Mazao yanashamiri
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.

9) Matatizo pia yapo, Kama vile maleria,
Gonjwa latupiga kumbo, Twahitaji kuliua,
Tutaja liweka kambo, Wote mkisaidia,
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.

10) Mwisho Twawakaribisha, Wawekezaji Nchini
Watalii mje ona, Nchi yetu hii nzuri,
Wote mliofika hapa, Muijue nchi hii,
Nchi yetu Tanzania, Twawakaribisha wote.
Pia watu mabali mbali waliomba kupiga picha kwa pamoja na waTanzania kama unavyoona

Thursday, October 11, 2007

GOVT ENDS TANESCO'S MONOPOLY

September 19, 2007
Posted by nchiume under Energy
New York
September 18th, 2007
Minister of Trade, Industry and Marketing, Hon. Basil Mramba, made what he termed as “the first official public announcement” that the Tanzanian Government will now allow private energy companies to distibute power in the country.
Speaking at the 2nd annual Tanzania Investment Forum in New York, Minister Mramba said that the move will effectively end TANESCO’s long held monopoly in power distribution. “From now on, any qualified company will be able to apply for licence to generate and sell electricity to the market”. Minister Mramba added that what remains is the official passage of the law which is currenty being prepared. The added that the amendment is expected to be tabled in the Bunge sometime this year in November at the earliest or by April of 2008.
Since early 1990’s, private power companies in the country have been generating their own electricity using gas and diesel fired turbines but were required by law to sell only to TANESCO, the Government owned power utility company. In recent years, few exemptions where given to mining and gas companies to generate and distribute power for their own use to support local operations. Today’s announcement, however, will open the field to more players from inside and outside the country to add power to the National grid and supplement TANESCO’s role of distributing electricity to urban and rural consumers. In recent years, due to various reasons such as economic and population growth as well as structural problems, TANESCO had been unable to cope with the rising demand for electricity in the market. For this reason, the liberalization of power distribution had been lobbied for a long time by the businesses and consumers alike as one of the panaceas to the power crisis in the country.
In other major news today, the board of directors of Millenium Challenge Corporation have approved a $698 million Millennium Challenge Compact to Tanzania to reduce poverty, stimulate economic growth, and increase household incomes through targeted infrastructure investments in transport, energy, and water.

Wednesday, October 10, 2007

ROSE MUHANDO TOGETHER WITH KANSAS CITY TANZANIANS AFTER SUNDAY SERVICE

To view a larger picture, click on the image and a new screen will pop up with an enlarged view (click kwenye picha)

IMF COMMENDS TANZANIA'S ECONOMIC PERFORMANCE 2007

By Mgeta Mganga
The International Monetary Fund (IMF) has commended the economic performance of Tanzania, saying it continues to be strong. Speaking to reporters in Dar es Salaam yesterday, an official from the IMF economic department, Roger Nord, said the improvement was fueled by a rebound in the agricultural sector and improved electricity supply. He also attributed the performance to the economic growth which stood at 6 percent in 2006/07. `The economic growth is on track. It is likely to exceed 7 percent in 2007/08,` he said. Nord led a four-man IMF delegation currently in the country to conduct the second review under the policy support instrument. Nord, however, said that the country was still facing two challenges, which include returning inflation to its downward trend. Inflation now stands at 10 per cent. He said the Bank of Tanzania intention to meet its target of reducing inflation was critical toward reducing high interest rates, supporting productive investment, growth and reducing poverty. `In this regard, we welcome the Bank of Tanzania’s efforts to strengthen monetary policy implementation`, he said. He said the second challenge was to ensure that the ambitious targets for revenue and expenditure in the 2007/08 budget were attained. The official said the added revenue rightly reflected the key priorities of the government to further increase social spending, while significantly scaling up infrastructural investment. Revenue performance in the first quarter of 2007/08 had been strong. Nord commended the TRA for strengthening tax administration. He said the mission supported efforts to improve further public financial management with the twin objectives of raising the efficiency of public spending while strengthening accountability. For her part, Minister for Finance Zakhia Meghji said the main factors that had led to increased government revenue were the on-going economic reforms. “We reformed TRA, tighten tax loopholes and widened the tax base,”she said.
SOURCE: Guardian

TANZANIA CONSUL UNVEILS $100 MILLION PROJECT

Swallehe Msuya , Mshale Senior Staff Writer
Published 10/05/2007 - 9:30 p.m. GMT
MINNEAPOLIS – An ambitious $100 million project dubbed “World Trade Center Great Lakes & Kilimanjaro International” is to be built in Northern Tanzania, an official said. Kjell Bergh, Tanzania’s Minnesota-based consul for trade and investment promotion, said three Tanzanian investors were involved in the project and would partner with the Tanzanian government.Speaking at the Pan African Trade and Investment Summit, a three-day conference at the University of Minnesota, Bergh said 5,000 acres of land had been set aside for the project. It will have a University complex, a conference center, hotel complex, a golf course and an enterprise-processing center for exports.About investment opportunities in Tanzania, the consul said since independence in 1961, Tanzania had gone from one of the 20 poorest countries in the world to one of the most promising. Quoting a recent African Competitiveness Report issued by Harvard University, “Tanzania topped the improvement index.” “A recent World Bank/IMF study showed the country as the most improved in terms of business climate,” Bergh said. The country’s committed investment in education has enabled the number of Universities in Tanzania to jump from one at independence to more than 20 today.“The creation of the Dar es Salaam Stock Exchange has helped revitalize the Tanzanian economy, generating fresh capital for established and emerging firms,” Bergh said. “Between 1990 and 2005, approximately $10.2 billion in foreign direct investment helped create 3,531 projects, creating more than 500,000 direct and indirect jobs”.In March, the World Association of Investment Promotion Agencies and the UN Conference on Trade and Development named the Tanzania Investment Center, the one-stop investment processing facility, the best in the world. The center assists investors in dealing with all government agencies and cutting red tape.In terms of foreign investment, $ 475 million was invested in Tanzania in 2006, mainly in the mining and tourism sectors. Direct foreign investment is projected to increase to $550 million.Investors are assured of the safety of their investments, as Tanzania is a member of Multilateral Investment Guarantee Agency and International Center for Settlement of Investment Disputes. The country further enjoys a peaceful and stable democratic form of government.

Tuesday, October 2, 2007

SERIKARI YA TANZANIA YAPANIA URAIA WA NCHI MBILI

Na Mobhare Matinyi, New York
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, amesema serikali itahakikisha sheria ya uraia wa nchi mbili inapitishwa kwa manufaa ya Watanzania na taifa na si vinginevyo.Akizungumza na baadhi ya Watanzania waliokutana naye mjini New York(Mary Mitchell, Mobhare Matinyi,Namtasha Ikaweba, Shaaban Mseba, Augustino Malinda, Yasin Njayagha,Miraji Malewa,na Deogratias Rutabana) wiki iliyopita katika hoteli ya Grand Hyatt, Waziri Membe alisema lengo la serikali ni kuwasaidia Watanzania na si kugawa uraia wa Tanzania kwa wageni wenye uraia wa nchi zao.Alisema haingii akilini ni kwa nini Mtanzania wa kuzaliwa anyang’anywe uraia wa Tanzania kwa kuwa amechukua uraia wa nchi nyingine kutafuta faida za kielimu, ajira au hata matibabu.“Ni kwa nini tumuadhibu huyu Mtanzania wa kuzaliwa kwa kuwa tu amechukua uraia wa nchi nyingine ili apate elimu ama ajira na kusaidia ndugu zake waliobaki Tanzania?” alihoji Waziri Membe.Waziri alisisitiza kuwa sheria hiyo itakapopitishwa haitatoa mwanya kwa kila mtu kuuvamia uraia wa Tanzania bali itawalinda Watanzania wanaotaka kuchukua uraia wa nchi za nje kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla.Akitoa mfano mmojawapo bila kutaja majina ya wahusika, Waziri Membe alisema anaifahamu familia moja ya Watanzania ambayo ililazimika kuchukua uraia wa Kanada kwa sababu za matibabu, na kwamba kuwanyang’anya uraia watu hawa ni kuwaadhibu bila kujali uhai wao.Alieleza kuwa familia hiyo ina watoto wawili ambao matibabu yao hugharimu dola 2,000 kwa kila mmoja kwa mwezi, na kwamba kwa kuchukua uraia wa Kanada, matibabu hayo yanakuwa bure. Alihoji je, ni haki kuwanyang’anya uraia wao wa Tanzania?Akitoa mfano wa manufaa yanayopatikana Ghana, Waziri Membe aliwaambia Watanzania hao kwamba ni muhimu kwa Tanzania kutumia raia wake walioko nje kwa manufaa ya taifa na siyo kuwabagua.“Mwaka jana pekee wananchi wa Ghana walioko nje waliingiza dola bilioni 2.5 kwa njia mbalimbali halali,” na akaongeza: “Taifa dogo kama Komoro, mwaka jana lilipata dola milioni 89 kutoka kwa wananchi wake walioko Ufaransa pekee.Akifafanua zaidi, Waziri Membe alisema wakati akiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kipindi kisichofikia miaka miwili, Tanzania ilitoa uraia kwa wageni 101 na kushangaa ni kwa nini Watanzania wa kuzaliwa wapoteze uraia wao.Waziri Membe aliwataka Watanzania kujenga umoja thabiti na kuwahakikishia kwamba serikali itakuwa pamoja nao ili kuleta maendeleo kwa taifa, na kwamba mawazo kuwa usalama wa taifa utakuwa hatarini si la jambo kuhofia iwapo sheria itatungwa vizuri.Tanzania ina raia wake waliosambaa nchi mbalimbali duniani huku idadi kubwa ikiwa katika nchi za Kiarabu za Ghuba ambako wakati serikali ikiongeza ofisi moja ya Ubalozi nchini Oman miaka michache iliyopita ilikadiria kuwa kuna Watanzania laki tano.Nchi nyingine ambazo Watanzania wanakadiriwa kuwa wengi ni za Marekani Kaskazini na Ulaya Magharibi ambako wako kwa maelfu, ambao wengi wao hukabiliwa pia na utata wa uraia wa watoto wao wanaozaliwa ugenini.Mjadala wa suala la uraia wa nchi mbili umekuwa ukiendelea nchini katika siku za karibuni ambako kumeibuka kambi za wanaopinga kwa madai ya kulinda maslahi ya nchi na wanaounga mkono kwa madai hayo hayo ya kulinda maslahi ya nchi.